1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaKorea Kaskazini

Korea Kaskazini haitaki mawasiliano yoyote na Japan (Kim Yo)

26 Machi 2024

Dadake kiongozi wa Korea Kaskazini mwenye ushawishi mkubwa, Kim Yo Jong, amesema Jumanne kuwa nchi hiyo itakataa mawasiliano au majadiliano yoyote na Japan.

https://p.dw.com/p/4e9Cs
Dadake Kim Jong Un asema Korea Kaskazini haitaki mawasiliano yoyote na Japan
Dadake Kim Jong Un asema Korea Kaskazini haitaki mawasiliano yoyote na JapanPicha: KCNA/AP Photo/picture alliance

Yo Jong ameyasema haya siku moja tu baada ya kudai kuwa Waziri Mkuu wa Japan Fumio Kishida, alikuwa ameomba kufanya mazungumzo na kakake Kim Jong Un.

Hapo jana Kim Yo Jong ambaye ni mmoja wa wasemaji wakuu wa utawala huo, alisema haiwezekani kufanyika mkutano na Japan hadi pale Tokyo itakapobadilisha sera yake kwa Korea Kaskazini.

Lakini leo amesema hatua ya Japan kukosa ujasiri kwa ajili ya mahusiano mapya ya Korea Kaskazini na Japan, ukiwemo msimamo wake kuhusiana na suala la utekaji nyara na mipango ya kijeshi ya Korea Kaskazini.

Kihistoria mahusiano ya nchi hizo mbili yameharibika kutokana na mzozo wa muda mrefu wa utekaji nyara na mipango ya kijeshi iliyopigwa marufuku ya Korea Kaskazini.

Katika siku za hivi karibuni lakini, Waziri Mkuu Kishida ameelezea nia ya kuyaboresha, jambo ambalo Pyongyang haikulipinga.