1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Muungano wa upinzani wa Ujerumani wajadili tena uhamiaji

10 Septemba 2024

Muungano wa vyama pinzani vya siasa za wastani za mrengo wa kulia nchini Ujerumani vya CDU/CSU, kwa mara nyingine unashiriki mazungumzo ya pamoja na serikali ya Kansela Olaf Scholz juu ya sera ya uhamiaji na usalama.

https://p.dw.com/p/4kTWQ
Ujerumani Solingen | Olaf Scholz
Viongozi waandamizi wa serikali nchini Ujerumani wakiweka mashada ya maua kwenye eneo kulikotokea shambulizi la kisu kwenye mji wa Solingen na kuibua mjadala kuhusu uhamiajiPicha: Thomas Banneyer/dpa/picture alliance

Mkutano huo unaofanyika mjini Berlin ni wa pili katika awamu ya mazungumzo yanayovihusisha vyama tofauti, tangu kulipotokea shambulizi la kisu katika mji wa Sollingen mwezi uliopita na kurejesha masuala ya uhamiaji katika ajenda za kisiasa.

Mkutano huo wa ngazi ya juu kuhusu uhamiaji unalenga kufafanua mkakati wa pamoja wa serikali.

Muungano wa upinzani wa CDU/CSU umeitaka serikali ya  Kansela Scholz inayoongozwa na chama cha siasa za wastani za mrengo wa shoto, kuanzisha hatua kali za kukabiliana na wahamiaji katika mipaka ya Ujerumani.

Hilo lilikuwa sharti la awali la kuendelea na mazungumzo zaidi.