1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ukosefu wa maji walazimisha Tembo kuihama Zimbabwe

19 Septemba 2023

Makundi makubwa ya Tembo wanaihama hifadhi kubwa ya wanyama pori nchini Zimbabwe na kuingia taifa jirani la Botswana wakitafuta maji, hali inayotishia kuongeza makabiliano kati ya watu na wanyamapori.

https://p.dw.com/p/4WUkz
Mnyama Tembo
Mabadiliko ya Tabianchi yanatajwa kuchangia kukauka kwa vyanzo vya maji kwenye mbuga za wanyama Picha: Zinyange Auntony/Getty Images

Hayo yameelezwa na msemaji wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa za Zimbabwe, Tinashe Farawo, ambaye amearifu kuwa Ndovu hao walianza kuhama tangu mwezi Agosti na wanaelekea nchini Botswana baada ya vyanzo vya maji kwenye mbuga ya wanyama ya Hwange nchini Zimbabwe.

Inaaminika sababu za kukauka kwa vyanzo vya maji ni athari za mabadiliko ya tabianchi.

Farawo amesema idadi ya tembo wanaohama ni kubwa na kuna mashaka watalazimika kupita kwenye maeneo yenye shughuli nyingi za binadamu.

Mwaka uliopita pekee tembo walisababisha vifo vya watu 60 nchini Zimbabwe, takwimu zinazoakisi ongezeko la muingiliano baina ya watu na wanyama hao wa mwituni.