1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiSudan Kusini

UN: Watu 700,000 waathiriwa na mafuriko Sudan Kusini

6 Septemba 2024

Ofisi ya Masuala ya Kibinaadamu ya Umoja wa Mataifa, OCHA, imesema zaidi ya watu 700,000 wameathiriwa na mafuriko kote Sudan Kusini na kuonya idadi ya walioathirika inaongezeka kila siku.

https://p.dw.com/p/4kNLD
Manusura anasaidiwa kupanda ukuta kufuatia mafuriko makubwa eneo la Tokar Kusini, Jimbo la Red Sea, Sudan
Manusura anasaidiwa kupanda ukuta kufuatia mafuriko makubwa eneo la Tokar Kusini, Jimbo la Red Sea, SudanPicha: El Tayeb Siddig/REUTERS

OCHA limesema mafuriko yamesababisha uharibifu mkubwa kwa nyumba, mazao na miundombinu muhimu, kuvuruga mfumo wa elimu na huduma za afya na kuongeza hatari ya milipuko ya magonjwa.

Soma pia: Takriban watu 30 wauawa baada ya kuporomoka kwa bwawa, Sudan 

Shirika hilo la Umoja wa Mataifa Iimesema kufikia Septemba 5, mafuriko yameathiri zaidi ya watu 710,000 katika kaunti 30 kati ya 78.

Mashirika ya misaada yameonya kuwa nchi hiyo inakabiliwa na mafuriko mabaya zaidi kuwahi kutokea katika miongo kadhaa na OCHA imesema wengi bado hawapati misaada wanayoihitaji.