1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Blinken awasili Cairo kushinikiza amani Mashariki ya kati

18 Septemba 2024

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken yuko mjini Cairo, wakati juhudi za kutafuta makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Hamas yakizidi kuwa magumu kufuatia wimbi la mashambulizi nchini Lebanon.

https://p.dw.com/p/4kks3
Misri | Antony Blinken huko Cairo
Waziri wa Mambo ya Nje Antony Blinken akiwasili kukutana na Rais wa Misri Abdel Fattah El-Sisi katika Ikulu ya Al-Ittihadiya mjini Cairo, Misri, Septemba 18, 2024.Picha: Evelyn Hockstein/REUTERS

Katika ziara yake ya kumi huko Mashariki ya Kati tangu kuanza kwa vita vya Gaza takribani mwaka mmoja uliopita, Blinken atajadili hatua hizo za upatanisho na maafisa wa Misri. Anatarajiwa kukutana na kiongozi wa taifa hilo Abdel Fattah al-Sisi na kufanya mkutano wa pamoja na waandishi habari na mwenzake wa Misri, Badr Abdelatty. 

Soma pia:Matumaini ya kusitisha mapigano Gaza yanafifia 

Hata hivyo, mara hii Blinken haitoitembelea Israel. Maafisa wa Marekani wanasema hawatarajii mengi makubwa katika mazungumzo yake lakini wanaamini  ziara yake itaendelea kuweka shinikizo kwa pande mbili hasimu, Israel na Hamas, kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano. 

Ziara yake inafanyika wakati msururu wa vifaa vya mawasiliano vinavyotumiwa na wanachama wa Hezbollah kuripuka katika maeneo kadhaa nchini Lebanon na kusababisha vifo vya watu tisa na kuwajeruhi wengine zaidi ya 2,800 katika shambulizi ambalo Hezbollah inadai limefanywa na Israel.